About Us



GET TO KNOW US
TUJUE ZAIDI:




Distinction Education centre (DEC) ni kituo binafsi cha kipekee mkoani DODOMA 
kinachotoa Elimu inayoendana na kasi na sera ya Wizara ya ELimu chini ya 
Walimu binafsi na wazoefu katika tasnia ya ufundishaji wa masomo ya Sayansi, 
sanaa na biashara. Distinction ni kituo kisichokuwa na mpinzani kwa ufundishaji 
na mafanikio ya wanafunzi mjini Dodoma. Kituo kina walimu wa kutosha kwa 
michepuo yote na mazingira mazuri ya mwanafunzi kusoma kama vile notes,
vitabu vya kiada na ziada, vifaa vya maabara, na eneo lenye utulivu kwa kujifunzia.
Kituo kipo Dodoma Mjini Mtaa wa UHINDINI mkabala na jengo la Vision Fund 
karibu na Maghorofa ya mwapwa flat (NHC)



LENGO LA KUANZISHA 
DISTINCTION EDUCATION CENTRE:

Kituo hiki kilianzishwa kwa lengo la kusaidia wanafunzi kuwawekea misingi bora katika masomo ya Sayansi, Hisabati, Sanaa na Biashara kupitia programu za tuisheni wakati wa likizo kwa wanafunzi wa bweni na kila siku jioni kwa wanafunzi wa shule za kutwa kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha sita.
Pia kuwasaidia wanafunzi katika maandalizi ya kurudia mitihani ya kidato cha nne na sita (Resiters) na Elimu ya sekondari kwa miaka miwili (QTs)

COORDINATORS: MASTER JOVIN AND SIR BANKA

Comments

Post a Comment